Wadau wa Sekta ya Asasi za Kiraia/Watetezi wa Haki za Binadamu tunapenda kutoa salamu za pole kwa Rais wetu, Mhe Rais Samia Suluhu kutokana na kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli. Aidha, kwa pamoja tumeendelea kuungana na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan pamoja, viongozi wengine wa serikali na watanzania wote kwa ujumla katika kuomboleza kifo cha Hayati Rais Magufuli. Wakati huo huo tunapenda kutumia fursa hii kumpongeza Mhe. Samia Suluhu kwa kupata nafasi ya kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
SALAMU ZA POLE KWA MH.RAIS SAMIA SULUHU HASAN